Wizara ya Afya Zanzibar imesema itaanza kuhamisha huduma za uzazi katika Hospitali ya Mnazi mmoja ili kuweza kupisha ujenzi

Wizara ya Afya Zanzibar imesema itaanza kuhamisha huduma za uzazi katika Hospitali ya Mnazi mmoja ili kuweza kupisha ujenzi, ukarabati na utanuzi wa Hospitali hiyo unaotarajiwa kuanza mwezi wa sita mwaka huu. Akitoa Taarifa kwa wananchi Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Hassan Khamis Hafidh amesema kutokana na kuanza kwa taratibu za utanuzi na ujenzi wa […]

Wizara ya Afya Zanzibar imesema itaendelea kushirikiana na Mashirika ya kimataifa kutokomeza Malaria Zanziabr

WIZARA ya Afya Zanzibar imesema itaendelea kushirikiana na Mashirika ya kimataifa na wadau wengine kuhakikisha kuwa maradhi ya Malaria yanaondoka hapa nchini. Akifungua Mkutano wa siku moja wa Mpango Kazi kwa mwaka 2025 uliowashirikisha Wadau na Mashirika ya Kimataifa   Mkurugenzi Kinga na Elimu ya Afya Wizara  ya Afya Zanzibar  Dkt Salim Slim amesema jitihada zinafanyika […]

Wanafunzi wa Skuli ya Maandalizi Kidutani wamepatiwa huduma za Upimaji wa Afya na madaktari kutoka China

JUMLA ya watoto 400 wa Skuli ya Maandalizi ya Kidutani wamepatiwa huduma ya upimaji wa afya ili kuhakikisha wanakuwa na afya njema. Zoezi hilo lililofanyika skuli hapo, liliendeshwa na timu ya Madakari wa Kujitolea kutoka China ambapo watoto hao walipatiwa uchunguzi tofauti ikiwemo upimaji wa macho, masikio, vinywa na shinikizo la damu. Akizungumza kwenye zoezi […]

Wizara ya afya Zanzibar imekabidhiwa sehemu ya ardhi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya cha Jimbo la Magomeni

Wizara ya afya Zanzibar imekabidhiwa  sehemu ya ardhi   yenye ukubwa wa mita za mraba 1564.12 katika eneo la magomeni kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya cha jimbo. Akizungumza katika makabidhiano hayo katika eneo la  kiwanja cha mpira wandarasi magomeni mkoa wa mjini magharibi, mkurugenzi mkuu wizara ya afya Zanzibar dr amour Suleiman mohammed […]

Wizara ya Afya Zanzibar imesema itafanya jitihada za makusudi kuhakikisha mawasiliano yanafanyika kwa maabara zote za Afya nchini

WIZARA ya Afya Zanzibar imesema itafanya jitihada za makusudi kuona kuwa mawasiliano yanafanyika kwa maabara za Afya na maabara nyengine hapa nchini kwa lengo la kukabiliana na magonjwa mbali mbali yakiwemo ya miripuko. Akizungumza katika mkutano wa kupitia Muongozo wa Maabara kwa wadau mbali mbali, Mkurugenzi Tiba wa Wizara ya Afya Zanzibar Dkt Marijan Msafiri […]

Wizara ya Afya Zanzibar imekabidhi kifaa cha kupumilia kinachojulikana kama Portable Oxygen kwa Bi Zahra Waziri Saidi

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Boharikuu ya Dawa Zanzibar(CMC) imekabidhi kifaa cha kupumilia kinachojulikana kama portable oxygen kwa Zahra Waziri Saidi anaesumbuliwa na ugonjwa wa kupooza viungo. Akikabidhi kifaa hicho naibu waziri wa afya Zanzibar Hassan Khamis Hafidh  amesema kuwa taarifa za kuhitaji kifaa hicho wamezipata kupitia mitandao ya kijamii na kuona ipo haja […]

Loading