WIZARA ya Afya Zanzibar inatarajia kufanya utafiti maalum wa kitaifa wa viashiria vya magonjwa yasiyoambukiza (NCD Steps Survey)

WIZARA ya Afya Zanzibar inatarajia kufanya utafiti maalum wa kitaifa wa viashiria vya magonjwa yasiyoambukiza (NCD Steps Syrvey) ifikapo Septemba 9 mwaka huu ikiwa na lengo la kuandaa mikakati ya kuona maradhi hayo yanapungua. Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Naibu waziri wa Afya Zanzibar, Hassan Khamis Hafidh, alisema, utafiti huo utagusa jumla ya kaya […]

Wizara ya Afya Zanzibar yatiliana saini mkataba wa mashirikiano na Taasisi ya Mkapa Foundation

WIZARA ya Afya Zanzibar imetiliana saini mkataba wa mashirikiano baina ya Benjamini Mkapa Foundation wa kuimarisha sekta ya afya hapa nchini. Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar Dkt Amour Suleiman Mohamed amesema mkataba huo utaimarisha ushirikiano wa utaoji wa huduma za afya katika nyanja tofauti ikiwemo ya rasilimali watu. Amesema Benjamini Mkapa Foundation imekuwa […]

Waziri wa Afya Zanzibar amepokea msaada wa vifaa vya Wamama Wajawazito kutoka Vodacom Tanzania Foundation

WAZIRI wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui amesema kuja kwa mradi wa Mmama utasaidia kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi hapa nchini. Akizungumza na waandhishi wa wa habari kuelekea uzinduzi wa kupatiwa vifaa vya mama wajawazito kupitia mradi wa Mmama vilivyotolewa na Vodacom Tanzania Foundation ambavyo vitatolewa huko Kizimkazi na Rais wa Jamuhuri wa Muungano wa […]

Wizara ya Afya Zanzibar Kuendeleza ushirikiano na UNICEF

WIZARA ya Afya Zanzibar imesema kuwa itaendelea kushirikiana na Shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia masuala ya watoto Duniani UNICEF katika kuimarisha huduma za Afya hapa nchini. Hayo yameelezwa na Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui wakati alipofanya mazungumzo na Mwakilishi mpya wa taasisi ya hifadhi ya watoto wa shirikika la umoja wa mataifa […]

Ziara ya Mh.Waziri kwenye vituo vya Afya Wilaya ya Kati na Mjini

WIZARA ya Afya Zanzibar imesema inakusudia kuimarisha huduma za afya ya msingi kwa kuweka mindombinu yenye ubora zaidi  na wananchi waendelee kupata matibabu bila ya usumbufu. Hayo yameelezwa na Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui katika muendelezo wa Ziara yake  ya kutembelea vituo vya afya aliyofanya Wilaya ya Kati na Mjini ya kuangalia miundombunu […]

WIZARA ya Afya Zanzibar Kuimarisha mashirikiano yake na Shirika la Afya Ulimwenguni WHO

WIZARA ya Afya Zanzibar imesema itaendeleza mashirikiano yake na Shirika la Afya Ulimwenguni WHO katika kuimarisha huduma za Afya hapa nchini. Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui amesema hayo huko ofisini kwake wakati alipomkaribisha Mwakilishi Mkaazi mpya wa Shirika la Afya ulimwenguni nchini Tanzania alipofika kwa kujitambulisha. Amesema WHO inafanya kazi kubwa hapa nchini […]

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar, imesema itaendelea kuimarisha huduma za afya ya msingi kwa maeneo yote ya Unguja na Pemba

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar, imesema itaendelea kuimarisha huduma za afya ya msingi kwa maeneo yote ya Unguja na Pemba ikiwa na lengo la kuboresha huduma za uzazi salama, matibabu ya meno na kinywa, uchunguzi wa ‘ultra sound” na huduma za maabara zipatikane kwa ufanisi wenye vituo vya afya vyote vya msingi kwa maeneo yote […]